
Wakizungumza na Mwanahabari wetu kwa maskitiko makubwa Baadhi ya
wananchi hao wamesema mbali na kuwaomba viongozi wao wa majimbo
kusimamia matengenezo ya Barabara hiyo lakini mpaka sasa hawajaona
matengenezo yoyote.
Wamesema kwa muda mrefu sasa wanapewa ahadi na viongozi wa serikali
pamoja na viongozi wa majimbo kuwa barabara hiyo itatengenezwa lakini
hawajaona matengenezo na kulazimika kushindwa kufanya shughuli zao za
maendeleo kijijini hapo.
Aidha wamesema kijiji hicho kinashindwa kukuwa kiuchumi kutokana na
wananchi wake kushindwa kusafirisha bidhaa wanazozalisha kupeleka
masokoni kutokana na ubovu wa barabara unaosababishia wamiliki wa magari
kushindwa kutoa huduma ya usafiri kwa uhakika.
Zaidi ya miaka kumi wananchi wa miwani wamekuwa wakilalamika tatizo
la ubovu wa barabara bila ya kupatiwa ufumbuzi na kuwasababishia
wananchi matatizo ikiwemo wajawazito kujifungulia njia.
chanzo:Zanzibar24.
Comments