Kaimu mkurugenzi wa mfuko huo makame mwadini silima akizungumza
wakati wakisaini makubaliano baina ya mfuko huo na benki ya posta
tanzania amesema pamoja na fursa hiyo ya kielimu makubaliano hayo pia
yanahusu mkopo kwa wanachama wa zssf wanaoanza maisha.
Amesema mfuko umelenga kuwanufaisha wanachama katika nyanja
mbalimbali huku akiahidi kutolewa elimu ili kuwafahamisha jinsi ya
kutumia fursa hiyo pamoja na masharti yanayohitajika ili kupata mikopo
hiyo.
Mkurugenzi mtendaji wa benki ya posta tanzania sabasaba mushingi
amesema benki inakusudia kutatua changamoto hasa kwa vijana wanaoanza
maisha baada ya kuajiriwa kwa kukosa huduma muhimu kutokana na kutokuwa
na fedha za kujiandaa na maisha.
Mkopo wa elimu utakaotolewa kwa wanachama wa mfuko huo ni kwa viwango
mbalimbali ikiwemo cheti hadi phd katika vyuo vya ndani na nje ya nchi.
chanzo:Zbc.
Comments