
Akizungumza na mwandishi wetu Mkuu wa Idara ya mazingira Pemba Mwalimu
Khamis Mwalimu amesema mafuta hayo yameenea katika eneo lenye ukubwa wa mita
200 hali ambayo inaweza kusababisha uchafuzi wa mazingira na kupoteza maisha ya
viumbe vya baharini.
Amesema kwa hatua ya awali kuna watu wameanza kuyafyoza
mafuta hayo kwa kutumia masponji ili kuepusha athari zaidi na kulinda mazingira
ya eneo hilo.
Akielezea chanzo cha kumwagika mafuta hayo nahodha wa meli
hiyo aliyejitambulisha kwa jina la MALBORO amesema meli hiyo ilifika salama
kutoka bandari ya Wete na taratibu zote za ukaguzi zifanyika laki mara baada ya
maji kutoka meli ili jigonga na jiwe na kuanza kumwaga mafuta.
Comments