Mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya Merck Dkt Rasha kelej ametoa kauli hiyo
baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan ikulu jijini dar es salaam
na kusema kuwa taasisi hiyo imejitolea kuisaidia Serikali ya Tanzania
katika jitihada zake za kuboresha sekta ya afya kwa Tanzania Bara na
Zanzibar kupitia mpango huo unaotarajiwa kuanzishwa mwishoni mwa mwaka
huu.
Dkt Rasha Kelej amesema mafunzo hayo kwa wataalamu wa afya yatatolewa
kwa muda wa mwaka mmoja hadi mitatu katika mataifa ya India, Ulaya na
Kenya lengo likiwa ni kuboresha upatikanaji wa huduma zote zinahusu
saratani hapa nchini.
Taasisi ya Merck pia imemhakikishia makamu wa Rais kuwa watajikita
katika kuwajengea uwezo akina mama wenye matatizo ya ugumba kwa
kuhakikisha wanapata taarifa sahihi zinazohusia na matatizo ya ugumba
hivyo itasaidia kubadilisha mtazamo ambao umejengeka kwenye jamii kuhusu
masuala ya ugumba kwa akina mama.
Ajenda hii itasimamiwa kupitia programu ya Merck more than a mother.
Aidha, makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan ameipongeza taasisi ya
merck kwa juhudi zao za kuboresha sekta ya afya Barani Africa na
amewakaribisha kufanya kazi nchini Tanzania.
Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan amesema amefurahishwa na mipango
na mikakati ya taasisi hiyo na kwamba Serikali iko tayari kushirikiana
na Merck Foundation katika kuwajengea uwezo kina mama pamoja na utoaji
wa mafunzo kwa wataalamu mbalimbali wa sekta ya afya nchini hasa kwenye
matatizo yaSaratani na ugumba kwa ujumla.
Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa watendaji wa taasisi hiyo
zinaonyesha kuwa tatizo la ugumba kwa wanandoa barani Africa ni kubwa
ambapo inakadiriwa kwamba katika kila ndoa nne, moja inasumbuliwa na
changamoto ya ugumba na karibu asilimia 85 ya ugumba inasababishwa na
ukosefu wa matibabu kwa magonjwa ambayo yanaweza kutibika.
chanzo:Zbc.
Comments