Tatizo la maji laikumba shehia ya kilombero.

Wananchi wa Jimbo la Kiwengwa  Shehia ya Kilombero Mkoa wa kaskazini  Unguja Wilaya ya kaskazini B wamelalamikia kuwepo kwa  tatizo la maji  katika maeneo  yao hali inayopelekea kutumia maji ya mito na visima ambayo hawana uhakika kwa usalama wa afya zao.

Akizungumza na Mwandishi wetu Katibu wa Sheha wa shehia ya Kilombero John Ndarami  Makeja amesema kukosekana  kwa huduma ya maji safi na salama  kunawapa wasiwasi mkubwa  kupata ugonjwa wa Mripuko kutokana na wananchi walio wengi  kutumia maji ambayo  hayapo salama kwa kunywa,kupikia pamoja  na kufanyia shughuli nyengine kwa mahitaji  ya  nyumbani.


Kwaupande wake Afisa Mamlaka ya Maji Zanzibar Zawa Zahor Suleiman Khatib amesema  kukosekana kwa huduma ya maji safi na salama katika shehia ya kilombero kuna sababishwa na  ubovu wa mashine pamoja na pampu yakupelekea maji katika mabomba.

Hata  hivyo Zahor ametoa wito kwa wananchi wa kilombero  kuwacha kutumia maji ya mito na visima visivyo na usalama  na badala yake kwenda kuchota maji katika maeneo jirani ili kunusuru wananchi kuugua ugonjwa wa kipindupindu wakati huku mamlaka  inaendelea na jitihada za kuitengeneza mashine  hiyo ili kurudisha huduma ya maji katika maeneo yao kama  awali.

Nae Mwakilishi wa Jimbo hilo la Kiwengwa Asha Abdalla Mussa amewataka wananchi wa kilombero kuwa na subra kwani  viongozi wa jimbo kwa kushirikiana na  Mamlaka  ya Maji zawa  wanalitafutia ufumbuzi tatizo hilo linalowakabili.

Hivi karibuni  Vijiji cha Kilombero kilikubwa na ugonjwa wa kipindupindu  kutokana na  matumizi ya maji yasio salama  kiafya.
chanzo: zanzibar24.

Comments