Soko kuu lateketea moto Zambia.

Soko kuu nchini Zambia limeteketea kwa moto na kuharibu tegemeo la wafanyabiashara wengi.Soko hilo la City Market lililo mjini Lusaka limekuwa likiteketea tangu mapema leo Jumanne.

Kwa upande wa msemaji wa polisi Esther Katongo na meya wa mji wa Lusaka Wilson Kalumba wanasema kuwa bado wanachunguza chanzo cha moto huo.


Wafanybiashara wengi wamefikwa na majonzi makubwa baada kupoteza mali yao.”Nitailisha vipi familia yangu kwa sabaua  ninategemea hapa,” alisema Loveness Banda huku akiangalia kutoka mbali soko likiteketea.

Miongoni mwa walioshuhudia tukio hilo wanasema kuwa moto huo ulisababishwa na hitilafu ya umeme na kuwalaumu wazima moto kwa kuchelewa kufika kuzuia moto huo kusambaa.

Soko hilo lina wafanyabiashara wengi zaidi nchini Zambia. Kati ya bidhaa zinazouuzwa ni pomoja na nguo za mitumba, vifaa vya elektroniki na hata vyakula.
 chanzo:zanzibar24.

Comments