
Hayo yamebainishwa na mkuu wa mkoa wa Mjini Ayoub Mohammed Mahmoud
wakati akizungumza na waandishi wa habari huko Ofisini kwake Vuga Mjini
Unguja.
Amesema hivi karibuni amefanya safari ya kuenda nchini Marekani ndani
ya kampuni inayodhibiti vitendo vya uhalifu duniani kwalengo la kuagiza
vifaa madhubuti vya uchunguzi yaani CCTV Camera kwa dhumuni la
kufikishwa nchini ili kuchungunguza matukio mbalimbali yanayofanyika
hapa nchini.
”Matumaini yaliopo mwezi ujao mwezi ujao vifaa vitaanza
kufanya kazi nchini”amesema Mh Ayoub.
Amesema kufuatia tukio lililo fanyika Daraja bovu Konda wa daladala
kupigwa mapanga kamati kamati maalumu ilijipanga kikamilifu kuwatafuta
wahalifu wa tukio hilo, tayari wamesha tiwa mikonononi mwa Serikali
ambao kwa idadi ni 44.
Hata hivyo Mh Ayoub ametoa indhari watu 336 waliobainika kuwa na
tabia ya vitendo vya uhalifu kufika vituoni wenyewe ndani ya wiki mbili
kuanzia Julai 30 kabla ya Serikali kuchukua hatua mikononni mmwake.
“Wazazi wa watoto wanajihusisha na vuitendo vya uhalifu kufikisha
taarifa kwenye vyombo vya sheria zawatoto wao la si hivyo tutawakamata
pamoja na watoto wao.”
Vile vile ametoa wito kwa wananchi kuwa kutokuwa na hofu ndani ya
mkoa wao kwani upo salama na waendelee kutoa taarifa ambapo tu tatizo
linapotokezea.
Ayoub ameviomba vikosi vya usalama nchini kuwa linapotokezea tukio
lolote ni wajibu kulifuatilia kwa haraka zaidi kwa wakati unaofaa.
chanzo: zanzibar24.
Comments