Smz kuendelea kuwasaidia wananchi wanao ishi ukanda wa pwani.

Serkali ya Mapinduzi Zanzibar imesema itaendelea kuwaondolea tatizo la ushafiri wananchi walioko katika sehem za visiwa, ikiwa ni mpango endelevu ulio andaliwa na serekali.

Hayo yameelewa leo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikowa na Idara Maalum Zanzibar Mh. Haji Omar Kheri wakati akikabidhi boti mbili na mashine zake kwa niaba ya Rais wa Zanzibar  na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar Dr Ali Mohd Shein kwa ajili ya kuondoa tatizo la ushafiri baina ya Kisiwa Panza na Chokocho Kisiwani Pemba.


Amesema mpango wa Serekali nikuhakikisha tatizo la usafiri katika visiwa vidogo vidogo vya unguja na pemba linamalizika kwa kupatiwa boti za kisasa kwa ajili ya kuuvuushiya.

Mh. Haji amefahamisha kuwa boti hizo zitatowa huduma bure kwa wananchi wa kijiji cha Chokocho - Kisiwa Panza na wananchi watatakiwa kidogo kwa ajili ya gharama za mafuta ambapo wiki moja kuanzia leo itakua ni bure.

Nae Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mh. Mwanajuma Majid Abdallah amepongeza juhudi za Serekali chini ya uwongozi wa Dr. Shein za kutatua kero za wananchi katika suala zima la usafiri walioko katika Visiwa na kuwataka  wananchi kuzitumia boti hizo bila ya ubaguzi.

Kwa upande wake kamanda wa kmk Zanzibar Nd. Hassan Mussa amesema pamoja na boti hizo kutumika kwa kuvuushia wananchi bali zitasaidia sana katika ulinzi hasa katika kipindi hichi cha uwokoaji wa zao la karafuu. 
 

Comments