MZEE WA MIAKA 70 AHUKUMIWA MIAKA MITANO JELA.

Mahakama ya mkoa mwera imemuhukumu kifungo cha miaka mitano mshitakiwa khalid juma hassan baada ya kupatikana na hatia ya kosa la kubaka.

Akisoma hukumu hiyo hakimu wa mahakama hiyo muhammed ali amesema adhabu hiyo imetolewa baada ya upande wa mashitaka kuthibitisha kosa dhidi ya mshitakiwa huyo.

Mshitakiwa huyo mkaazi wa muyuni c mwenye umri wa miaka 70,
ambae ni mjomba wa mtoto aliyefanyiwa ukatili huo, pia ametakiwa kulipa faini ya shilingi milioni 20 na akishindwa atumikie tena chuo cha mafunzo miaka miwili na kufanya muda wa kifungo kuwa miaka saba.

Hakimu huyo amemtaka mshitakiwa kulipa fidia ya shilingi milioni tano kwa mtoto huyo mwenye umri wa miaka kumi na nne.

Awali baada ya mahakama kumtia hatiani mshitakiwa huyo upande wa mashitaka unaongozwa na mwanasheria kutoka ofisi ya mkurugenzi wa mashitaka ( dpp) uliiomba mahakama kutoa adhabu kali kutokana na vitendo hivyo kukithiri katika jamii.

Kwa upande wa wakili wa utetezi wa mshitakiwa huyo shaibu ibrahim aliiomba mahakama kutoa adhabu kwa mshitakiwa huyo ya kutumikia jamii kutokana na kuwa na umri mkubwa na hali yake ya kiafya sio nzuri.

ilidaiwa mahakamani hapo kuwa mnamo tarehe 20 mwezi wa 11 mwaka jana mshitakiwa khalid juma huko mutuni c alimuingilia mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 14, ambapo jumla ya mashahidi 6 waliweza kutoa ushahidi wao mahakamani hapo..
chanzo:Zbc.

Comments