
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Semina ya siku moja ya ukusanyaji
mapato kwa kutumia Mashine za kielekroniki (EFDs) kwa Wakuu wa
Mikoa,Wilaya na Makatibu tawala wa Mikoa na Wakurugenzi wa Manispaa
amesema nchi nyingi zinakuwa kimaendeleo kutokana na kufanikiwa
kuhifadhi mapato ya kodi.
Hata hivyo amesema wakusanyaji kodi watakapo fanya kazi kwa uadilifu
na kufuata sheria wataisaidia serikali kutekeleza azma yake ya kufikia
malengo waliyoyakusudia katika mwaka wa Fedha 2017/18 pamoja na
kuwakamata wafanya biashara wote wanaokwepa kulipa kodi.
Akizungumzia matumizi ya Mashine hizo za EFD hapa Zanzibar, amesema
mashine hizo zitasaidia kuondoa udanganyifu katika kulipa kodi kwa
wafanyabiashara na kukusanya Fedha zilizokusudiwa kwa wakati na kutoa
wito kwa wafanyabiashara kuendeleza utamaduni wa kulipa kodi ili nchi
iweze kupiga hatua kimaendeleo.
Kwa upande wake Meneja wa Sera, Utafiti na Mipango wa ZRB Ahmed Haji
Saadati amesema mbali na Mashine hizo kuhifadhi mapato yasipotee lakini
pia zitasaidia kutunza kumbukumbu za mauzo na manunuzi kwa wafanya
bishara ili kuondoa matatizo yanayoweza kujitokeza ikiwemo ukwepaji wa
kodi kisheria.
Nao washiriki wa mkutano huo wameahidi kufikisha elimu hiyo kwa
wananchi walio katika shehia zao ili wananchi waweze kunufaika na kodi
wanazotoa kwa kutekelezewa mahitaji muhimu ikiwemo Elimu, Afya na
Miundombinu bora ya barabara.
Mashine hizo za EFD zinataraiwa kutumika hapa Zanzibar ifikapo mwezi
November ili kuimarisha mapato yatokanayo na wananchi ikiwemo wafanya
biashara kwa lengo la kuimarisha maendeleo ya nchi.
chanzo:zanzibar24.
Comments