MKURUGENZI WA MASHTAKA ZANZIBAR ( DPP) AKIZUNGUMZA UWASILISHAJI WA RIPOTI YA UENDESHAJI WA KESI ZA UDHALILISHAJI.
Akizungumza katika uwasilishaji wa ripoti ya operesheni ya uendeshaji
wa kesi za udhalilishaji mbele ya waandishi wa habari katika ofisi ya
Mkurugenzi wa mashataka iliyopo uwanja wa Matumbaku amesema,operesheni
hiyo ya awamu ya kwanza iliyoanzia Tarehe 01.3.2017
imewezesha ofisi
hiyo kupeleka Majalada 55 katika Mahakama mbali mbali za Unguja na
hatimae kuwezesha kesi 53 kati ya hizo kusikilizwa na nyengine kutolewa
hukumu ndani ya kipindi kifupi.
Mbali na hilo mkuregenzi wa mashtaka amekemea baadhi ya makadhi
wanaotoa vyeti feki vya ndoa kwamba kufanya hivyo ni kosa la jinai na
kuwatahadharisha kwamba kuanzia sasa atakaebainika kufanya udanganyifu
huo atashtakiwa kwa kosa la kuidanganya serikali.
Aidha Dpp aliziomba taasisi zinazojishughulisha na haki jinai
kuzidisha mashirikiano ya pamoja kama ambavyo wameanza kupitia
operesheni hizo maalum walizozianzisha ili kusukuma mwenendo wa kesi za
udhalilishaji ziende kwa haraka ili kuona tatizo hilo linamalizika.
Mkutano huo wa dpp na waandishi wa habari juu ya kutambulisha
uzinduzi wa operesheni ya uendeshaji wa kesi hizo kwa awamu ya kwanza na
ya pili umekenda sambamba na kuwataka wananchi kujitokeza kutoa ushahidi
wa kesi za udhalilishaji kwani kwani bila ya ushahidi ofisi ya
muendesha mashtaka haitaweza kupeleka majalada mahakamani na hatimae
wananchi watailaumu serikali wakati wakosa ni wao wananchi.
chanzo:Zbc.
Comments