Wizara ya Miundombinu ,mawasiliano na uchukuzi imeanza ujenzi wa
barabara ya kizimbani hadi kiboje kwa kiwango cha fusi ili
kuwaondolea wananchi usumbufu unaokwamisha shughuli zao za
maendeleo.
Wakizungumza na Waandishi wa Habari, Wananchi pamoja na Viongozi wa
Jimbo la miwani wamesema ujenzi wa barabara utaweza kuleta faraja
waliokuwa wanaitafuta kwa muda mrefu kwani tatizo la barabara
hiyo ilipelekea kusitisha shughuli zao mbalimbali za
kiuchumi pamoja na kukosekana kwa daladala za abiria.
Kwaupande wake Katibu Mkuu Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano
Mustafa Jumbe amesema tayari serikali imeshaanza hatua za awali za
kuitengeneza barabara hiyo kwa kiwango cha fusi ili kurahisisha huduma
za usafiri kwa wananchi.
Amesema pia kukamilika kwa barabara hiyo kutawawezesha wananchi
kusafirisha mazao wanayozalisha kijijini hapo pamoja na kurahisisha
huduma nyengine za kijamii ikiwemo upatikanaji huduma za hospital
zilizositishwa kutokana na ubovu wa barabara hiyo.
Barabara hiyo inatarajiwa kukamilika hivi karibuni kwa kiwango cha
kifusi ambayo inaurefu wa kilomita 7.5 kutoka kizimbani, miwani hadi
kiboje.
chanzo: Zanzibar24
Comments