MAHKAMA YA MWANAKWEREKWE IMEWAPANDISHA WASHTAKIWA KWA MAKOSA YA UZALILISHAJI.

Mahkama ya wilaya mwanakwerekwe imewapandisha k vya mahkama hiyo washtakiwa kwa makosa ya uzalilishaji ambayo yamekuwa kilio kikubwa kwa jamii hivi sasa.

Washtakiwa hao ambao kesi zao zimefikishwa mbele ya hakimu mdhamini wa mahkama hiyo muhammed amour, hakimu fatma muhsin, na hakimu chausiku kafuti kuya, chini ya waendesha mashtaka arafa zubeir, sara omar na saidi ally.

Washtakiwa hao nipamoja na aliye tuhumiwa kumtorosha mtoto aliyechini ya uwangalizi wa wazazi wake,
mtuhuhumiwa aliyemkashifu mschana bila ya ridha yake jambo ambalo nikosa kisheria pamoja na mtuhumiwa aliyemchukua mtoto mwenye umri wa miaka mitano na kumpeleka katika boma na kumkashifu.

Watuhumiwa hao waliiyomba mahkama kuwapatia dhamana ombi ambalo halikukubaliwa na kesi zao kupangwa tarehe nyengine
 chanzo:Zbc.

Comments