Maalim Seif awatowa wasi wasi wanachama wa CUF.

maaalimBaraza kuu la uongozi ngazi ya taifa la chama cha wananchi CUF Zanzibar limesema haliwatumbuwi wanachama walioteuliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC hivi karibuni kutokana na kutofata sheria za chama hicho.

Akizungumza na waandishi wa Habari  katika ofisi za chama hicho Vuga Mjini Zanzanzibar ,Katibu Mkuu wa Chama cha wananchi CUF Maalim Seif Sharif Hamadi amesema kwa mujibu wa sheria na katiba ya Chama hicho wabunge ni lazima watambulike na baraza hilo ndipo kutangwazwa na tume ya Uchaguzi.


Maalim Seif amesema Baraza hilo litaendelea kuwatambua wanachama hao kutokana na kuwa ni wanachama halali wanaotambulika kisheria, licha ya kuwa tume ya Uchaguzi imesha tangaza majina mapya yatayoweza kujaza nafasi zilizoachwa wazi na wanachama waliofukuzwa.

Amesema mbali na wabunge hao baraza hilo pia litaendelea kuwatambuwa madiwani wa Viti maaalum  akiwemo Mh. Leila Hussein Madibi anaetokea Ubongo  na Elisabeth Mangwanja anaetokea Temeke licha ya kuwekewa vikwazo vya kutotambuliwa na uongozi wa Prof. Ibrahim Lipumba ambao ni feki na hautambuliki kisheria.

Aidha Baraza hilo limesema litaendelea kuwaunga mkono wananchama hao katika kutafuta haki yao ya msingi kwa hatua ya kupeleka malalamiko yao mahakamani ili waweze kuwatumikia wananchi katika keleta maendeo ya nchi na Chama hicho.

Maalimu Seif ametowa wito kwa Jumuiya za kimataifa kuiwekea vikwazo vya kiuchumi Tanzania pamoja na kuitenga kisiasa na kidiplomasia hadi watawala watakapo heshimu haki za binaadamu na utawala wa sheria.

Hata hivyo amewatowa wasi wasi wanachama wa CUF kuendelea kukiunga mokono chama hivyo ili kiweze kuwaletea maendeleo katika nchi.
chanzo:Zanzibar24.

Comments