Kichanga chaokotwa kwenye jaa la taka Darajabovu.

Image result for daraja bovu unguja.Mtoto mchanga wa kiume anayekadiria kuwa ni wa ujauzito wa miezi saba ameokotwa akiwa ameshafariki dunia katika jaa la taka Darajabovu Redio One wilaya ya Magharibi A Unguja.

Kwa mujibu wa sheha wa shehia hiyo Mohammed Ameir Khamis amesema, tukio hilo limetokea jana Julai 17, 2017 majira ya saa moja asubuhi baada ya watoto waaliokuwa wakiokota chupa kukikuta kichanga hicho katika jaa hilo.


Kamanda wa polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Kamishna msaidizi mwandamizi wa polisi Hassan Nassir Ali akithibitisha kutokea kwa tukio hilo amesema: “maiti hiyo imetupwa jaani na mtu asiyejulikana na ilipelekwa hospital ya Mnazi mmoja uchunguzi wa daktari umefanyika na upelelezi wa polisi unaendelea”.

Aidha Kamanda Hassan amewataka wazazi kuacha tabia hizo zisizokuwa za kiuungwana.
 chanzo:zanzibar24.

Comments