Akizungumza katika Sherehe ya kumbukumbu za kuadhimisha Miaka 60 ya
Mstahahiki Karim Agakhan Mwenyekiti wa Ismailia Agakhan Zanzibar
Zulfikar Bhaloo amesema Jumuiya yao imekuwa mstari wa mbele kusaidia
jamii katika nchi mbalimbali duniani kwa kutoa huduma za
maendeleo ikiwemo sekta ya Afya,Elimu, na usaidizi wa kutengeneza
mazingira bora ya kujitengemea katika miradi ya maendeleo.
Hata hivyo Bhaloo amesema Jumuiya hiyo ikisaidia miradi mengi ya
maendeleo nchini Zanzibar ikiwemo Miradi ya elimu salama mtoto kwa
mtoto,Mradi wa bustani ya forodhani na Mradi wa Hoteli ya Zanzibar
Serena ambao unachangia mapato katika mfuko mkuu wa serikali na
kuwataka wananchi kuvienzi vitu hivyo ili viwe histori kwa zanzibar.
Mapema akifungua sherehe hizo Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharib Ayoub
Mohammed Mahmoud amesema Mstahahiki Karim Agakhan alitoa mchango mkubwa
Zanzibar ambao umeleta maendeleo na kuinua uchumi wa watu wa
zanziabr.
Amesema Zanzibar bado inahitaji wawekezaji kuwekeza Zanzibar ili
kusaidia kukuza na kuinua uchumi wa nchini kwalengo la kuleta
maendeleo.
Sherehe hizo pia ziliambatana na uzinduzi wa Nembo ya kumbukumbu
ya miaka 60 ya Uongozi wa Shekh Karim Agakhan ambayo ilizinduliwa na
mkuu wa mkoa wa mjini magharibi Ayoub Mahmoud.
chanzo:zanzibar24.
Comments