
Akizungumza na Zanzibar24 huko ofisini kwake Madema Mjini Zanzibar
Kamanda wa Polisi Mkowa wa Mjini Hassan Nassir amesema kumejitokeza
baadhi vya vikundi vinavyojihusisha na wizi katika maeneo mbali mbali ya
Zanzibar jambo linalowatia hasara kubwa wafugaji.
Amesema katika kukomesha vitendo hivyo Jeshi la polisi katika Wilaya
ya Magharib A na B tayari linaendelea na hatua ya kuvitafuta vikundi
hivyo ambapo kwa sasa Baadhi ya wahusika wa wizi wa mifugo
wameshakamatwa.
”tumeanza kupeleleza ni nani anaefanya vitendo hivi na kuna
washtakiwa wachache wamesha kamatwa pale Fuoni na kuna kazi kubwa
tunafanya na karibuni wizi huu utaisha nako huko maungani tatizo hilo
lipo mda mrefu na mpaka sasa washtakiwa tumesha wakamata, sasa hawa wa
fuoni nao tutawakamata wananchi watulie na waendeleee kutupa taarifa”
Aidha kamanda Nassir ametowa wito kwa jamii kuendelea kuwa waangalifu
juu ya mifugo yao pamoja na kuacha tabia ya kujichukulia hatua mikononi
mwao pindipo watawakamata wizi hao jambo ambalo ni kinyume na taratibu
zilizowekwa .
chanzo:zanzibar24.
Comments