IGP Sirro ziarani Pemba: Ahimiza umoja na upendo miongoni mwao.

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro, amefanya ziara ya kikazi katika mkoa wa kusini Pemba, huku akiwataka askari kufanyakazi katika misingi ya ueledi na uzalendo na kuhakikisha kuwa vitendo vya uhalifu na wahalifu vinakomeshwa.

Hayo ameyasema huko kisiwani Pemba alipo, kuwa  katika  kikao kazi na watendaji wa Jeshi la Polisi wa mikoa miwili ya Pemba yenye lengo la  kujitambulisha toka aliposhika nafasi ya kuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini na kuchukua nafasi ya mtangulizi wake ambaye ni Mkuu wa Jeshi mstaafu Ernest Mangu.


IGP Sirro amesema kuwa, katika hatua za kukabiliana na matukio ya kihalifu ikiwamo biashara haramu ya kusambaza na kuuza dawa za kulevya ni vyema Askari kote nchini  wakatimiza wajibu wao kwa kufuata misingi ya sheria na taratibu.

Alisema katika awamuyake ya uwongozi amedhamiria kuona kila askari anapenda kazi na kutumia muda mwingi katika kutekeleza majukumu yao na kuhimiza umoja upendo na mashirikiano miongoni mwao.

Alisema mgawanyo wa idara zlizomo ndani ya jeshi hilo hazifanyi askari kujiona bora na kumdharau mwengine bali kila askari anawajibu wa kujenga mashirikiano na mwenzake ilikuhakikisha lengo la jeshi la polisi la ulinzi wa raia na mali zao  linafikiwa.

Mapema Mkuu huyo wa Jeshi la Polisi alifika ofisi ya Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba  na kujitambulisha Mbele ya wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama kisiwani Pemba.

Aidha aliihakikishia kamati hiyo kuwa, Jeshi la Polisi nchini litahakikisha linaendelea kudumisha hali ya ulinzi na usalama kwa mashirikiano makubwa na kuwapongeza kwa kuendelea kukifanya kisiwa cha Pemba kuwa katika hali ya amani na utulivu mkubwa.
chanzo: zanzibar24.

Comments