
Dk. Shein aliyasema hayo leo Ikulu mjini Zanzibar wakati alipokutana
na uongozi wa Wizara ya Biashara, Viwanda na Masoko, Bodi ya Wakurugenzi
ya Shirika la Biashara la Taifa la Zanzibar (ZSTC) pamoja na uongozi
wake.
Katika maelezo yake, Dk. Shein alitumia fursa hiyo kutoa pongezi kwa
Shirika la (ZSTC), kwa mafanikio makubwa iliyoyapata tokea kuanzishwa
kwa mabadiliko makubwa ikiwa ni pamoja na kutunga Sheria ya Shirika la
Biashara la Taifa Zanzibar (ZSTC) Namba 11 ya mwaka 2011 na ile Sheria
ya Maendeleo ya karafuu Namba 2 ya mwaka 2014.
Dk. Shein alieleza kuwa azma ya Serikali ya kurekebisha vituo vya
kununua karafuu vya ZSTC sambamba na kuimarisha miundombinu ya barabara
kwa maeneo yanayozalisha karafuu kwa wingi ni miongoni mwa hatua muhimu
za kuliimarisha zao hilo na kukuza bishara ya karafuu.
Alieleza kuwepo Sheria hizo ndani ya Shirika hilo zitalisaidia katika
kufikia lengo la kuimarika kwa biashara ya karafuu pamoja na biashara
nyenginezo ambazo zina maslahi na wananchi huku wananchi na wauzaji wa
karafuu nao wakiendelea kufaidika.
Aidha, Dk. Shein alieleza haja ya kuimarishwa mashirikiano kati ya
Bodi, Uongozi na Waziri ili Shirika hilo lizidi kuimarika sambamba na
kuendelea na kasi yake ya utendaji huku akieleza kuwa Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kuwaenzi wakulima wa karafuu kwa
kutambua kuwa biashara hio sio hasara bali ni faida.
Katika maelezo yake, Dk. Shein alisema kuwa ndani ya (ZSTC) mapato
yanaonekana na Shirika linakopesheka kutokana na mafanikio makubwa
iliyoyapata hivyo liendelee na kasi yake kwani uongozi wa Bodi na Wizara
uliopo una weza kuleta mabadiliko na maendeleo makubwa.
Sambamba na hayo, Dk. Shein aliutaka uongozi wa (ZSTC) kutambua kuwa
maghala yote ya Shirika hilo yaliopo Unguja na Pemba ni mali yao hivyo
ni lazima wayasimamie vyema na kuyatunza kwani sheria imewaruhusu.
Nae Makamo wa Pili wa Rais, Balozi Seif Ali Idd, alitoa pongezi kwa
Shirika hilo kwan kuendelea kufanya vizuri na kueleza haja ya kuendelea
kufanya vizuri kwani ni shirika la zamani na lina historia yake.
Waziri wa Wizara ya Biashara, Viwanda na Masoko Balozi Amina Salum
Ali alisema kuwa Shirika hilo ni miongoni mwa mashirika yaliopata
mafanikio makubwa nchini Tanzania ambalo halijawahi kupata misuko suko
hatua ambayo imetokana na miongozo mizuri ya Rais Dk. Shein.
Balozi Amina alieleza kuwa masoko ya bidhaa zinazozalishwa na ZSTC
yapo hata nje ya nchi na kusisitiza haja ya kuongeza uzalishaji wa
bidhaa kwa kuwashirikisha wakulima pamoja na vijana kulima mazao ya
biashara yakiwemo viungo huku akieleza uwezekano wa kuzalisha asali,
mbazi na dengu badala ya karafuu peke yake.
Aidha uongozi wa ZSTC ulieleza changamoto zilizopo sambamba na
mafanikio yaliopatikana huku ukieleza hatua zilizopatikana za mafanikio
kwa kupata mununuzi wa bidhaa za kwianda cha makonyo kutoka nchini China
ambaye ameahidi kunua bidhaa hizo tani 40 kila mwezi.
Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi Dk. Abdulhamid
Yahya Mzee alieleza haja ya kukiangalia kwa mtazamo wa uzalishaji wenye
tija kiwanda cha makonyo kilichopo Wawi kwa kukifanyia ukarabati ama
kukijenga upya ikiwa ni pamoja na kuweka mashine za kisasa kwa lengo la
kuweza kuzalisha bidhaa kwa wingi.
Mapema Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Biashara la
Taifa la Zanzibar (ZSTC) Kassim Maalim Suleiman, alieleza kuwa Shirika
hilo bado linaenda vizuri na limeweza kupata mafanikio makubwa licha ya
changamoto zilizokuwepo.
Mwenyekiti huyo alisifu mashirikiano makubwa yaliopo kati ya Bodi na
uongozi wa Wizara huku akieleza miongoni mwa mafanikio yaliopatikana
ikiwa ni pamoja na kuwa na hakiba ya TZS Bilioni 5.2 kuanzia Julai mwaka
2016 hadi Machi 2017.
Aidha, Mwenyekiti huyo alisema kwa mwaka huo wa 2016 hadi 2017
Shirika limeuza karafuu tani 2156 zenye thamani ya TZS Bilioni 36.6 huku
akieleza haja ya kutotegemea zao loa karafuu peke na badala yake
kutafuta mazao mengine ambayo yatalipunguzia mzigo zao hilo.
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk.
chanzo: zanzibar24.
Comments