Dalali wakike anaesambaza dawa za kulevya atiwa mbaroni, Unguja.

Dalali wa kike anaye husika na usambazaji wa dawa za kulevya kwa vijana amekamatwa na polisi wanaosimamia masuala mazima ya kupambana na dawa za kulevya nchini.

Mwanamke huyo anaejulikana kwa jina la Bi. Nuru Saleh Mzee mwenye miaka 54 mkaazi wa Kwaalinatu mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, amekamatwa na  kete 108  za unga unaoaminika kuwa ni dawa za kulevya  wakati alipokuwa katika harakati za usambazaji wa dawa hizo kwa Vijana.


Kwa upande wake mkuu wa kitengo cha kupambana na dawa za kulevya Mrakibu wa Polisi Omar Khamiss amesema jeshi la polisi limejipanga vikali kupambana na watumiaji na wasambazaji wa dawa za kulevya na teari  kuna kesi nyingi wameshazifikisha mahakamani.

“kuna kundi kubwa la vijana wanasema teari wamejirudisha katika hali ya kawaida lakini bado naamini kwamba ili wabaki salama basi dawa za kulevya ziwe hazipo nchini” alisema polisi huyo.
Hivyo mtuhumiwa huyo atafikishwa mahakamani mara baada ya taratibu zitakapo kamilika.

chanzo: zanzibar24.

Comments