Baraza la manispaa ya mjini limeagizwa kuiondosha gereji iliopo katika eneo la skuli ya lumumba.

Baraza  la manispaa  ya  mjini  limeagizwa  kuiondosha  gereji  iliopo  katika  eneo  la  skuli  ya  lumumba  kutokana kuleta usumbufu kwa wanafunzi na walimu.

Mkuu  wa  wilaya  ya  mjini  marina  joel  thomas  amesema  uwepo   wa  gereji  hiyo kunasababisha  hata uchafunzi wa kianzio cha maji na  mtaro  uliopo eneo la skuli.

Naibu  mkurugenzi  baraza  la  manispaa  ya  mjini  ali  abdalla  natepe amesema baraza limepanga kulitumia eneo hilo kwa  shughuli nyengine  ili kuepusha  athari.


Mwalimu  mkuu  wa  skuli  ya  lumumba  mussa  hassan  ameelezea  kutoridhishwa na hali iliyopo katika eneo hilo kutokana na kuwatia hofu huku vijana wanaofanyakazi katika gereji  hiyo  wakiomba kupatiwa mazingira  bora  ya  kuendeleza  shughuli  zao za  kujipatia  kipato.

 chanzo:Zbc.

Comments