
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei alisema mauaji
hayo yalifanyika juzi saa sita eneo la Kijiji cha Chingholwe, Kata ya
Chanjale, Tarafa ya Nongwe.
Kamanda Matei alisema chanzo cha tukio hilo ilidaiwa ni wivu wa
mapenzi na hata hivyo alisema chanzo halisi kilichosababisha mume huyo
kuchukua uamuzi wa kumchoma mkewe na kitu chenye ncha kali kifuani,
hakijafahamika na uchunguzi zaidi unaendelea na hatua za kumfikisha
mtuhumiwa mahakamani zitafuatwa.
chanzo: zanzibar24.
Comments