
Maafisa wa upelelezi wameeleza kuwa hawakukuta kaburi lake Zanzibar na waliambiwa kuwa anaishi Canada.
Awali kabla ya hukumu wawili hao walikubali kula njama na kuidanganya taasisi ya bima ya Scottish widows.
Aidha katika shauri hilo, Mahakama ilielezwa kwamba Arafa (48)
alipunguza madeni yenye thamani ya £80,000 kabla ya kusafiri kwenda
Zanzibar, ambapo ilisemekana amefariki katika ajali ya gari mwezi april
mwaka jana.
Pia Mahakama hiyo ilielezwa kuwa Bi. Arafa ambaye aliingia nchini
uingereza akitokea kenya 1998 kama mkimbizi, ana madeni na kampuni za
fenicha za BrightHouse na PerfectHome.
Mwendesha mashtaka Jonathan Barker aliiambia mahakama hiyo kuwa Bi.
Arafa alijiunga na bima ya maisha kwa jina la awali mnao mwaka 2013,
huku akimuweka mwanawe huyo kama mrithi. Na kama wangefanikiwa basi
wangelipwa £136,000, alisema Barker
Katika madai hayo ya uongo ilielezwa kuwa Bi. Arafa alifariki
kutokana na majeraha ya kichwani na kuambatanishwa cheti cha kifo chenye
tarehe 14 April.
Baada ya hapo wapelelezi wa shirika la Bima walisafiri kuja Zanzibar
na waligundua kuwa daktari anaetajwa kumtibu Bi. Arafa hakuwa kazini
siku iliyotajwa kufariki kwake.
Bi. Arafa alirudi Uingereza kwa ndege ya Emirates na alisafiri kwenda
Canada baada ya kuzungumza na simu na mwanawe akiwa Uingereza.
Mwendesha mashtaka huyo alimaliza kwa kusema “Bi. Arafa ndie kiongozi wa njama hizi na alimhusisha mwanawe”
chanzo:zanzibar24.
Comments