Zao la kahawa hatarini kutoweka duniani.

Watafiti kutoka Kew Gardens,London wanasema kuwa Wanywaji wa kahawa huenda wakapata kahawa isiyo na ladha nzuri na bei yake kuwa juu, kwani ongezeko la joto duniani linasababisha ardhi ambayo inaweza kutumiwa kukuza kahawa kupungua.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Kahawa Duniani Dkt Tim Schilling ameeleza kuwa katika baadhi ya maeneo ya uzalishaji wa kahawa, viwango vya joto vimeongezeka kiasi kwamba tayari viwango vya ubora wa kahawa vimeanza kuathirika.


Uzalishaji wa kahawa bora duniani bila shaka unakabiliwa na changamoto tele kutokana  na mabadiliko ya tabia nchi, magonjwa na wadudu, mahitaji mengine ya mashamba, upungufu wa wafanyikazi bila kusahau kuimarika kwa idadi ya wanywaji wa kahawa duniani kila mwaka”,anaongeza Dkt Schilling.

Kupanda kwa kiwango cha joto kwa nyuzijoto 3C kumesababisha kuongezeka kwa kiwango cha mvua kwa 15% haswa katika maeneo yanayokuzwa kahawa kwa kiwango cha juu mno ya Minas Gerais na Sao Paolo. Hali hii inaweza kusababisha kupungua kwa eneo zima linalokuzwa kahawa kutoka kwa 70-75% hadi 20-25%.

Ikiwa uzalishaji wa kahawa Ethiopia, kitovu cha kahawa ya hali ya juu ya Arabica, na pia taifa linaloongoza kwa uuzaji nje wa kahawa Afrika, huenda ukawa hatarini sana katika karne ijayo, hatua zisipochukuliwa.

Nchini Ethiopia na kwa kweli kote duniani, hatua zisipochukuliwa kahawa itapungua, na kuna uwezekano mkubwa ladha yake pia itakuwa mbaya na kugharimu zaidi,” Dkt Aaron Davis, mtafiti wa kahawa katika Kew na mmoja wa waandishi wa ripoti hiyo.

Wakulima maeneo ya mashariki ya nchi hiyo, ambapo mabadiliko ya tabia nchi tayari yanaathiri uzalishaji, wametatizika miaka ya karibuni, na wengi kwa sasa wanasema mavuno yameshuka kutokana na ukame wa muda mrefu.

Jamal Kassim, Mkulima wa kahawa Ethiopia, ameshuhudia upungufu mkubwa wa mazao yake tangu aipande miaka kumi iliyopita.

Miti yangu ilizaa matunda mengi sana katika miaka ya kwanza lakini sasa haizai tena. Nashindwa kukidhi mahitaji ya jamii yangu,” anasema.

Unywaji wa kahawa unatarajiwa kuzidi uzalishaji kwa mwaka wa tatu mtawalia, kwa mujibu wa takwimu kutoka kwa Shirikisho la Kimataifa la Kahawa (ICO). 

Kwa sasa, ni shehena ya kahawa iliyohifadhiwa kutoka kwa miaka ya nyuma ya uzalishaji kwa wingi ambayo imezuia kutokea kwa uhaba wa kahawa au kupanda kwa bei.

 chanzo:zanzibar24.

Comments