Wizara ya elimu yachangia ujenzi wa madarasa.

baraza-la-wawakilishiWizara ya elimu na mafunzo ya amali Zanzibar  imesema idadi kubwa  ya wanafunzi madarasani inachangiwa na upungufu na uhaba wa madarasa kwa baadhi ya skuli hadi kufikia wanafunzi 100 kukaa darasa moja.

Akijibu swali la msingi lililoulizwa  na wawakilishi Jaku Hashim Ayoub,Hidaya Ali Makame  na Hassan Khamis Hafidh Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mmanga Mjengo Mjawiri  amesema Serikali kwa kuliona tatizo hilo imeanza  kuchukua  jitihada mbalimbali katika kuhakikisha wanaimarisha mazingira ya watoto kujisomea, ili kuweza kupunguza  idadi  kubwa ya wanafunzi katika madarasa  ili kupata elimu katika mazingira bora kwa maendeleo yao.


Amesema miongoni mwa jitihada hizo ni kuhamasisha jamii kupitia kamati za skuli,kusaidia ujenzi wa madarasa  ambapo  jitihada za jamii imeanza kuonekana ambapo jumla ya madarasa 285 yamejengwa katika ngazi ya gebo na kukabidhiwa wizara kwa ajili ya kuyamaliza,jambo linaloitia ari serikali kuyamaliza kwa haraka.

Hata hivyo amesema  serikali  imekuwa ikijenga mahusiano mazuri na wahisani mbalimbali wa ndani na nje  ya nchi wakiwemo Zanzibar milele Foundation ,Serikali ya watu wa China, Shirika la mswaada wa Sweeden, ili kusaidia  tatizo la madarasa linalowakabili  kwa muda mrefu.

Aidha  amesema katika mwaka  2017/2018 Wizara imetenga jumla ya fedha billion 2,000,000,000 na bilioni 2 za wahisani, ili kusaidia uwendelezaji wa miundombinu wa sekta ya elimu, ambapo fedha hizo zitatumika kukamilisha jumla ya madarasa 200.
chanzo: zanzibar24.

Comments