Mkuu wa kitengo cha lishe
Pemba Nd.Raya Mkoko Hassan amewataka wazazi na walezi kuwapeleka watoto wao
kuanzia miezi 6 hadi miaka 5 katika vituo vya afya vilivyo karibu nao ili kupatiwa matone ya vitamen A,
vidonge vya minyoo pamoja na kupima afya zao ili kuwakinga na maradhi
yanayoweza kuwakumba watoto katika umri huo.
Ameyasema hayo leo alipokua akizungumza na waandishi
wa habari katika ukumbi wa jamuhuri hall uliopo Wete mkoa wa kaskazini ikiwa ni
muendelezo wa mwezi wa lishe ya mtoto na kuwataka kushirikiana kwa pamoja kutoa
elimu kwa jamii ili kuona zoezi hilo linafanikiwa kwa kiwango kinachohitajika.
Mkuu huyo amesema licha ya juhudi
zinazochukuliwa na kitengo hicho ikiwa ni pamoja na kufanya mikutano maeneo
tofauti lakini bado wananchi hawajakuwa na muamko juu ya masuala hayo.
Mkoko amefahamisha kuwa matone ya vitamen A humkinga mtoto na maradhi
mbali mbali kama utapiamlo, kupofuka kwa macho
na maradhi mengineyo ambayo ni
hatarishi kwa afya yake.
Aidha amesema kuwa zoezi hilo hufanyika kwa
mwaka mara mbili ikiwa ni kila baada ya miezi sita hivyo ni vyema wazazi
kufikisha watoto wao bila ya kukosa.
Kwa upande wake Afisa wa kitengo cha lishe
Pemba Nd. Massoud Omar Mohd amesema wapo
wanajamii wanaosema kuwa matone hayo yanakata uzazina kudai hilo sio kweli na
kuwataka kuachana na dhana hiyo aliodai kuwa nipotofu.
Comments