Wakulima wa Mpunga Bonde la Mjumbe Kangagani Pemba watarajio mazuri ya mavuno kulinganisha na misimu iliopita.

Wakitoa maelezo juu ya kufurahishwa kwao kutokana na kupata
mbegu bora za kisasa huko Kangagani, Wilaya ya Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba.
Wakulimahao, wamesema kwa sasa hawahitaji kurudi nyuma katika
masuala ya kilimo walichozoea na kurithi kwa wazee wao, bali wataendelea na
ukulima wa muda mfupi ambao utawaondolea kero ya kujikimu kwa chakula kwa
wakati.
Mmoja kati ya wakulima wa Mpunga katika bonde hilo, Time Bakar
Hassan, amesema kuwa wamepata tofauti kubwa ya uotaji na uzalishaji wa mpunga
baada ya kupatiwa mbegu za muda mfupi na kufuata maelekezo ya wataalamu.
Sambamba na hayo, Mwahaji Suleiman Haji, amesema kuwa, wataalamu
wa masuala ya kilimo imefikia pahala stahiki kupewa pongezi kwa kuwasaidia kwa
karibu mbinu bora za uzalishaji ambazo zitachangia katika kuwakwamua na ukali
wa maisha.
Kwa upande wake, Khamis Zuber Kassim, amewashauri wakulima
wenzake kufuata maelekezo wanayopatiwa na wataalamu wa masuala ya kilimo, ili
waweze kupata mabadiliko ya haraka yenye tija kwa faida yao.
Hata Hivyo ameiomba Idara husika kuendelea kutoa taaluma
inayokwenda na wakati, kila muda unaporuhusu, ili kuwasaidia kupata mavuno
mazuri.
Nae Afisa Mkuu Idara ya Umwagiliji Maji, Mbarouk Ali Mgau,
Amesema kuwa tofauti ya mapato ya mavuno yatakuwa mazuri kulinganisha na wakati
uliopita kwa wakulima waliokubali mabadiliko .
Aidha amewataka wakulima kufuta ushauri na mbinu wanazopatiwa na
wataalamu kulinganisha na hali ya hewa wanaweza kukomboka kiuchumi kwa kupata
mafanikio zaidi.
Comments