Tanzania imesikitishwa na marufuku ya uuzaji gesi Kenya.

Serikali ya  Jamhuri ya Muungano ya Tanzania imelalamika kutokana na hatua ya Kenya kupiga marufuku  wafanyabiashara wa Tanzania kuuza gesi ya kupikia nchini humo.

malalamiko hayo yamebainishwa na  katibu wa kudumu wa wizara ya biashara na uwekezaji Profesa Adolf Mkenda kuwa serikali  ya tanzania imegundua katazo hilo kupitia vyombo vya habari mjini Nairobi kwamba Kenya imepiga marufuku uingizwaji wa gesi ya kupika kutoka Tanzania kupitia mpaka wa Kenya na Tanzania.


Amesema kufanya hivyo ni  kinyume na makubaliano ya jamii ya Afrika mashariki na makubaliano waliyoafikiana baina ya Kenya na Tanzania   baada ya Kenya  kuiwekea marufuku Tanzania mnamo mwezi Mei 18, 2017.

Aidha  Profesa Mkenda amesema  hatua hiyo ya Kenya itaathiri wafanyibiashara  na raia wa kawaida wanaoendesha maisha yao  kupitia biashara ya kuuza gesi .

Amesema katika  mkutano wa Jamii ya Afrika mashariki  ulio fanyika mwezi juni 2- 2017 ulio wakutanisha pamoja  mawaziri wa biashara na viwanda  iliamuliwa  kwamba Kenya ilifaa kuondoa marufuku ili kuafikia makubaliano hayo ya Afrika mashariki.

kwa wakati huo  Kenya ilikubali kuondoa marufuku hiyo ya ununuzi wa gesi kutoka Tanzania kupitia mpaka wa mataifa hayo mawili.

Hivyo Profesa Mkenda amesema kuwa serikali ya Tanzania  itaendelea na mpango wa kutatua tatizo hilo.

Kwa upande wake  katibu maalum nchini Kenya Andrew Kamau amesema kupitia   gazeti la The Citizen nchini Tanzania, Siku ya Jumatatu limeandika  amesema  kuwa wafanyibiashara hawataruhusiwa kununua gesi kupitia mipakani katika kipindi cha juma moja.

Amesema hatua hiyo inalenga  kuzuia kampuni haramu zinazouza gesi ambazo zimeathiri usalama wa taifa hilo.
Chanzo:zanzibar24.

Comments