SMZ yatakiwa kuchukua jukumu la kuhifadhi mbegu za zao la mwani.

Wizara ya kilimo, Maliasili, Mifugo na uvuvi Zanzibar imetakiwa kuwa na utaratibu wa kuhifazi mbegu za zao la mwani ili kuwarahisishia wakulima kuwa na mbegu za hakiba wakati wa kiangazi na mvua.

Akizungumza na mwanahabari wetu  juu ya hatua za kuchukuwa wakulima ili zao hilo liweze kuwanufaisha wananchi katika kipindi cha mvua na kiangazi mtafifi wa sayansi ya bahari Dk.Flower Ezekiel Msuya amesema wakulima wanashindwa kuendelea na kilimo kutokana na mwani kuharibika na kupelekea kukosa mbegu za kuendelea na kilimo hicho.


Amesema pindipo serikali itachukuwa jukumu la kuhifadhi mbegu hizo zitasaidia kwa kiasi kikubwa kuwawezesha wakulima kuzalisha mwani unaolingana na mahitaji ya soko na kuweza kuleta maendeleo ya haraka katika Nchi.

Kwa upande wake Afisa Mupango kutoka shirika la Maendeleo ya Viwanda ya Umoja wa taifa kutoka (UNIDO) Gerald Runyoro wa amesema watashirikikana na serikali katika kutafutia masoko ya zao hilo ili wakulima waweze kunufaika na bei nzuri zinazotokana na bidhaa wanzozalisha pamoja na kutowa wito kwa watafiti hao , kuwa na utaratibu wa kufanya utafiti katika mazao ya baharini ili wakulima waweze kukabiliana na athari zinazoweza kujitokeza.

Akifunga mkutano huo wa siku mbili Naibu katibu mkuu wa wizara ya kilimo ,Dk.Islam Seif amewataka wakulima wa mwani kufuata taratibu za kiafya walizopangiwa ili waweze kulima mwani wenye ubora  wakati serikali ikiendelea na kufanya tathmini juu ya kuyapatia ufumbuzi wa muda mrefu maradhi yalivamia zao la mwani.
chanzo:Zanzibar24.

Comments