
Aidha Waziri Haroun aliongeza kuwa endapo kiongozi ataepuka kujaza au
kufanya udanganyifu wowote katika fomu hiyo atachukuliwa hatua za
kisheria, huku tayari jumla ya fomu 1600 zimepokelewa.
Akizungumzia kuhusiana na Rushwa pamoja na uhujumu wa uchumi, Waziri
Haroun amesema katika kesi za rushwa na uhujumu wa uchumi Zanzibar kwa
makosa mbalimbali yakiwemo yakupokea rushwa, matumizi mabaya ya ofisi na
mali za umma pamoja na kukwepa kulipa kodi mamlaka imefanya udhibiti
na kugundua makosa 71 ambapo majalada 11 yapo kwa DDP na 4 yapo
mahakamani.
chanzo:Zanzibar24
Comments