Miswada miwili iliyo pitishwa na wajumbe wa baraza la wawakilishi leo.

wawkilishiWajumbe wa Baraza la Wawakilishi wamepitisha Miswada miwili ikiwemo Mswada wa sheria ya ushuru wa Stempu na Mswada wa Sheria wa ushuru wa bidhaa iliyowasilishwa katika kikao cha baraza la wawakilishi iyowasilishwa na Waziri wa Fedha na mipango Dk.Khalid Salum Mohamed.

Akisoma hutuba ya mswada wa sheria ya ushuru wa Bidhaa Dk.khalid amesema mswada huo utaimarisha mazingira ya uwekezaji Nchini kwa kuondoa utata juu ya mamlaka ya usimamizi ,utoaji na ukusanyaji wa ushuru.


Amesema mswada huo pia utalinda na kuongeza mapato ya serikali yanayotokana na vyanzio husika pamoja na kuwa na msingi thabit wa kisheria wa usimamizi wa ushuru huo na kuwepo ushuru wa kulinda hali ya kijamii na uhumi wa Zanzibar.

Akizungumzia Mswada wa sheria ya ushuru wa Stempu itakayochukuwa Nafasi ya sheria wa ushuru wa stempu NAM 6 ya Mwaka 1996 Waziri Khalid amesema mswada huo umegawika katika sehemu tano utaoweza kutoa fursa kwa wafanya biashara wadogo kulipia kodi kwenye taasisi moja ya ZRB.

Hata hivyo amesema mswada huo pia utaeka utaratibu bora na viwango maalumu vya kodi kwa wafanya biashara wadogo wa bidhaa na huduma na usimamizi wa ukusanyaji kodi kwa wafanya biashara waliokuwa hawakusajiliwa kwa viwango vya VAT.

Kwa kipindi kirefu wafanya biashara Wadogo walikuwa wakilalamikia gharama za ulipaji kwa kutakiwa kilipia kodi katika taasisi mbili na ukubwa wa kodi ambapo mswada huo utawasaidia kutatua matatizo yanayowakabili.
chanzo;Zanzibar24.

Comments