
Ameyaeleza hayo katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa mkoa wa kusini
Pemba, muda mfupi mara baada ya Mkuu wa mkoa huo Mwanajuma Majid
Abdallah, kumuapisha kushika majukumu yake, kufuatia uteuzi wake
uliofanya na rais wa Zanzibar DK. Ali M. Shein Juni 19 mwaka huu.
Alisema, ni vyema viongozi wenzake kuonesha ushirikiano kama vile
kumkosoa, kumuelekeza na kumuonyesha njia sahihi ili kufanikisha vyema
majukumu yake ya kuwatumikia wananchi na kutekeleza Ilani ya CCM ya
mwaka 2015/2020 kwenye nafasi yake hiyo.
“Mimi bado mdogo kwenye uongozi jamani,
sasa lazima mnishauri, mnielekeze, mniambie na muniite mkiona naenda
kombo, mkifanya hivyo lengo la Rais kuniteua litafikiwa”,alisema.
Mapema Mkuu wa Mkoa huo, Mwanajuma Majid Abdalla, alisema Rais
hakukosea kumteua Katibu tawala huyo, kutokana na umahiri wake kwenye
kazi.
Alisema, kwa vile anamfahamu vyema Katibu tawala huyo, anaamini
hakutakuwa na kazi kubwa ya kumuelekeza kwenye nafasi yake hiyo mpya.
“Mimi naamini, mkuu wa wilaya ya Mkoani Hemed Suleiman
Abdalla, hatokuwa na kazi kubwa sana kwa Katibu tawala wake, maana
anaweza na anafundishika”,alieleza.
Kwa upande wake, Katib Tawala Mkoa wa Kusuini Pemba Yussuf Mohamed
Ali, alimtaka Katibu tawala huyo wa wilaya ya Mkoani, kubisha hodi kila
mara kwenye ofisi yake, ikiwa atahitaji maelekezo.
Mkuu wa wilaya ya Mkoani Hemed Suleiman Abdalla, alimueleza Katib
tawala huyo, kukubali kufundishwa, kuelekezwa na kukosolewa, ikiwa ni
njia moja wapo ya kuelekea mafanikio.
Aidha Hemed, alimueleza Katibu huyo, kwa vile anaongoza jamii kubwa
ya watu, ajue kuwa, atakumbana na vikwazo, makero, shida, watu
kutomkufahamu ingawa yote hayo ni sehemu ya uongozi.
Rais wa Zanzibar na Mwneyekiti wa baraza la Mapinduzi
Zanzibar Mhe: dk Ali Mohamed Shein, kwa kutumia kifungu cha 15 (1,2,na
3) sheria no 8 ya mwaka 2014 ya Tawala za Mikoa alifanya utezi wa
viongozi mbali mbali, akiwemo Katibu tawala wilaya ya Mkoani Miza Hassan
Faki.
chanzo: zanzibar24.
Comments