Jeshi la polisi mkoa wa kusini Pemba lasema kifo cha aliyekuwa mwanafunzi wa shule ya Laurent Intanational School iliyopo Ole Kianga hakikutokana na kupigwa na mwalimu kama inavyodaiwa.

Image result for nembo ya jeshi la polisi tanzaniaKamanda wa jeshi la polisi mkoa wa kusini Pemba Mh, Sheikhan Mohd Sheikhan amesema kifo cha Saleh Abdallah Massoud  aliyekuwa mwanafunzi wa shule ya Laurent Intanational School iliyopo Ole Kianga Mkoa wa Kusini Pemba  hakikutokana na kupigwa na mwalimu kama inavyodaiwa na walio wengi bali kimechangiwa na kuumwa na Figo, Ini pamoja na uvimbe  katika shingo yake.

Akizungumza na wandishi wa habari huko ofisini kwake Madungu Chake Chake Pemba amesema kuwa  mnamo tarehe 30/05/2017 majira ya saa 5;00 asubuhi walipokea taarifa  ya kifo cha mwanafunzi huyo na ndipo wakachukua hatua za haraka kufika shuleni hapo kuhoji walimu pamoja na wanafunzi wa shule hiyo na  katika taarifa za awali uchanguzi huo ulibaini kwambo mwanafunzi huyo alipata adhabu baada ya kuharibu midoli ya kufundishia wanafunzi wa chekechea shuleni hapo.


Shekhan amesema,kabla ya hapo awali alipata kuanguka  chooni na kuumia sehemu ya bega la mkono wa kulia na alianza kupatiwa matibabu ya awalii na daktari wa shule hata hivyo hali haikua nzuri na kulazimika kupelekwa hospitali ya Chake Chake na Mwanamashungi kwa matibabu zaidi.

Amefahamisha kuwa 25/05/2017 baba wa mtoto huyo alifika shulenio hapo kwa ajili ya kumchukua na kwenda nae nyumbani kwa lengo la kumpeleka hospitali ya Wete kwa matibabu zaidi aliruhusiwa kurudi nae nyumbani na ilipofika 29/05/2017 alirejeshwa tena hspitali ya wete na kulazwa na hatimae majira ya saa08;00 alifariki dunia.

Amesema kuwa kutokana na uchnguzi wa daktari  aliyemtibu  katika hospitali ya Wete aligundua kuvimba kwa shvu la kulia ,uvimbe usio na maumivu mbeleni mwa shingo, uvimbe kwenye mguu wa kulia,umanjano wa macho yake  na hakua na jeraha lolote wala sehemu yeyote iliyotoka damu wala mkwaruzo au alama zisizo za kawaida.

Pia vipimo vingine vilionesha  kuwa alikuwa na upungufu wa damu ,kuumwa na Figo pamoja na Ini na sio kujeruhiwa  na kupelekea hali yake kuwa mbaya na hatimae kufariki dunia.

Aidha amesema kwa sasa wanawashikilia watu saba na uchunguzi ukikamilika watapandishwa mahakamani kwa kujibu shtaka la uzalilishaji pomoja na uzembe na sio shtaka la mauaji.

Comments