Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula
alitoa kauli hiyo wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Maswa
Mashariki, Stanislaus Nyongo (CCM). Nyongoa alitaka kujua serikali ina
mpango gani wa kulialika NHC kujenga nyumba katika mkoa mzima wa Simiyu.
Mabula alisema hadi sasa halmashauri mbili za Busega na Bariadi ndizo
zimetenga maeneo kwa ajili ya NHC kujenga nyumba, na zinazobaki
zinatakiwa kutenga maeneo, kuwalipa fidia wananchi wenye maeneo na
kuweka miundombinu ili kujenga nyumba hizo.
Alisema halmashauri hizo
zinatakiwa kuwa na uhakika wa matumizi ya nyumba hizo, kwani kuna
halmashauri 30 ambazo zimejengwa nyumba na NHC na hazitumiki.
Akijibu swali la msingi la Mbunge wa Itilima, Njalu Silanga (CCM)
aliyetaka kujua ni lini ahadi ya Rais ya wakati wa Kampeni mwaka 2015
itatekelezwa ya kujenga za watumishi katika wilaya ya Itilima, Naibu
Waziri, Ofisi ya Rais (Tamisemi), Selemani Jafo alisema katika mwaka
2017/18, serikali imetenga Sh milioni 250 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba
nne za watumishi.
“Katika mwaka wa fedha 2016/17, serikali ilitenga Sh milioni 230 kwa
ajili ya ujenzi wa nyumba nne za watumishi,” alisema. Aidha, serikali
imetoa Sh milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa ofisi ya Mkurugenzi
Mtendaji na ujenzi wake unatekelezwa na Wakala wa Majengo Tanzania
(TBA).
chanzo:Habarileo.
Comments