Dkt. Shein afanya uteuzi wa viongozi 7 katika Taasisi mbalimbali.

Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein amefanya uteuzi wa viongozi katika Taasisi mbalimbali za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Katika Uteuzi huo Dkt. Shein amewateua  Bw. Haji  Hamduni Omar kuwa Naibu Kamishna wa Chuo cha Mafunzo, Luteni Kanali Mussa Mohamed Shaame kuwa Mkuu wa Utawala wa Jeshi la Kujenga Uchumi (JKU) na Bw. Abdi Omar Maalim kuwa mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi Shirika la Meli na uwakala.


Aidha Dkt. Shein amewateua Bw. Hassan Abdalla Rashid kuwa Katibu tawala wa wilaya ya micheweni na Bi. Miza Hassan Faki kuwa katibu tawala wilaya ya mkoani .

Wengine ni Dkt. Juma Mohamed Salum kuwa Naibu Mkurugenzi Idara Habari Maelezo katika Wizara ya Habari Utamaduni Utalii na Michezo na Kanali Ali Hassan Hamad kuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo katika wizara ya Kilimo maliasili mifugo na Uvivu.

Uteuzi huo umeanza mara moja.
chanzo: zanzibar24.

Comments