
Balozi Seif aliyasema hayo chukwani nje kidogo ya Mji wa Zanzibar
kwenye ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar wakati akitoa hoja ya
kuahirisha Mkutano wa Sita wa Baraza la Tisa.
Akizungumzia kuhusu suala la mchanga Makamu wa Pili wa Rais wa
Zanzibar alisema hatua iliyo chukuliwa na serikali ilikua na dhamaira
yakuweka utaratibu mzuri wa matumizi bora ya rasilimli hiyo ambapo Jamii
inapaswa kuelewa kuwa kadri inavyotumika kwa kasi rasilmali hiyo ndivyo
inavyoendelea kumalizika.
Alisema Serikali haina nia ya kuwadhulumu Wananchi wake licha ya
kuwepo malalamiko mengi ya Baadhi waliokuwa wakimiliki maeneo ya vitalu
vya mchanga wakidai kuchukuliwa maeneo yao.
Hata hivyo Balozi Seif amewataka Wananchi wenye madai ya kuchukuliwa
maeneo yao ya vitalu vya Mchanga wawasilishe vielelezo vyao katika
Taasisi husika na aliwaahidi kero zao kufanyiwa kazi kwa mujibu wa
sheria na taratibu zilizopo.
chanzo: zanzibar24.
Comments