JESHI la Polisi linamshikilia kijana wa miaka 28 aliedaiwa
kumuingilia ndugu yake wa mama mmoja mwenye umri wa miaka 23 wakati
akiwa anakoga chooni.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini
Magharibi, Hassan Nassir Ali, alisema tukio hilo lilitokea Juni 26
mwaka huu saa 5.00 asubuhi Migombani mjini Unguja.
Alisema kijana huyo (jina limehifadhiwa) wakati mama yao akiwa
ametoka yeye na ndugu zake wengine kuelekea sokoni, ndipo ndugu
aliebakia nae nyumbani aliamua kwenda chooni kukoga na wakati akiwa
anaendelea kukoga, mtuhumiwa aliingia chooni na kumkamata kwa nguvu na
kasha kumuingilia.
Alisema baada ya mama yao kurejea, muathirika alimuhadthia mama yake
ndipo walipoamua kwenda kituo cha polisi Madema kutoa taarifa na
mtuhumiwa akatiwa nguvuni.
Kamanda Nassir, alisema kitendo kilichofanywa na kijana huyo ni cha
kinyama na kwamba atafikishwa mahakamani baada ya ushahidi kukamilika.
Aliwaomba wazazi na walezi kuwa na usimamizi mzuri katika familia zao
hasa kwa watoto ili kuwaepusha na matatizo yasiyokuwa ya lazima.
“Jambo la msingi wazazi kuwa karibu na watoto wao ili kuepusha vitendo na madhara ya udhalilishaji wa kijinsia,” alisema.
Chanzo: Zanzibar Leo na zanzibariyetu.
Comments