Hayo yamebainishwa leo na
Afisa Mdhamini Wizara ya ardhi mazingira
maji na nishati Mh.Juma Bakari Alawi katika uzinduzi wa uchimbaji wa mtaro wenye
lengo la kupeleka huduma hiyo katika hospitali ya Chake Chake .
Alawi amesema kuwa ZAWA
kupitia wataalamu wake katika kutafuta
njia ya kupata maji ili kuihudumia hospitali hiyo wameamua kukiimarisha kisima kilichopo
Madungu zstc ili kitoe huduma hiyo hospitalini hapo tu.
Aidha amesema jumla ya
shilingi Milioni 40 na laki nane za
kitanzania zitatumika kukamilisha mradi
huo ambazo fedha hizo zimeombwa kutoka kwa mshirika wa maendeleo ambaye ni
taasisi ya WATER FALLS ambayo makao makuu yake
yapo nchini Uingereza.
Amelezea kua uchimbaji wa
mtaro, ulazaji wa mabomba 7 ya nchi tatu,
ununuzi wa 'Pump' na ujenzi wa Wellhead inategemewa sana katika kipindi cha
wiki mbili kazi hizi itakua zimekamilika.
Hivyo amewaomba mafundi na wataalamu wa ZAWA kuipa umuhimu
kazi hiyo ili isichelewe zaidi ya muda
uliopangwa kukamilika.
Awali akimkaribisha mgeni
rasmi Afisa uhusiano wa mamlaka hiyo Nd.Suleiman Anas Massoud amesema ZAWA
imejizatiti kutokomeza ukosefu wa upatikanaji huduma ya maji safi na salama
katika maenee yote mijini na vijijini.
Kwa upande wake mkuu wa idara
ya ufundi wa mamlaka hiyo Nd, Juma Ali
Othman amesema kisima hicho kitatoa hudama massa 24 hospitalini hapo pamoja na eneo la madungu katika nyumba za Madaktari.
Amesema kuwa ni marufuku kwa
watu wa kawaida kuunga maji katika paipu
hizo kwani watakapounga watapunguza nguvu ya utoaji wa huduma katika maeneo hayo.
Comments