Zanzibar kuweka kituo cha kuhifadhia nyaraka na kumbukumbu za mambo yakale.

Image result for zanzibarZanzibar inatarajia kuweka kituo kikubwa na cha kisasa cha kuhifadhia nyaraka na kumbukumbu za mambo yakale  kwa faida ya sasa na kizazi kijacho.

Hayo yameelezwa na Naibu katibu mkuu wizara ya katiba sheria  utumishi wa umma na utawala bora Seif Shaaban Mwinyi kwenye hafla ya makabidhiano ya jengo jipya ambalo lilifanyiwa ukarabati mkubwa na kampuni ya ransi na kugharimu zaidi y a sh milioni 200.

Alisema kituo hicho kinatarajia kujengwa koani ambapo tayari serekali ya mapinduzi Zanzibar imekwisha wapatia taasisi yao ya nyaraka kiwanja na hatua ya sasa nikutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa jingo hilo.


Alisema kwa hivi sasa tayari wamekwisha fanya mazungumzo na nchi tafauti kama vile oman na irani ambapo wanasubiri wakati mipango ya kutafuta nji nyengine inafanywa nahata michoro ya kituo hicho ipo tayari.

Alisema kupatikana kwa jingo hilo kisiwani Pemba ni hatua muhimu katika azma ya taasisi kuwa na kituo bora cha kutunzia kumbumbu kwani kwa muda sasa Zanzibar inakabiliwa na tatizo la kituo cha kutunzia kumbukumbu.

Mapema wakati wa kumkaribisha naibu katibu mkuu huyo Afisa mdhamini wizara ya katiba sheria  na utumishi wa umma Masoud Ali Mohamed alisema kuhifadhi nyaraka na kumbukumbu nimuhimu kwa sasa na baadae na hivyo kuwataka watunza kumbukumbu kuzienzi ili ziweze kusaidia vizazi vinavyo kuja.

Kwa upandewake engenia alie lifanyia ukarabati huo kutoka kampuni ya ranscold   Mohamed Shehe aliitaka wizara walio ikabidhi jingo hilo kulikabua na kulifanyia ukarabati mara kwa mara ili liweze kudumu kwa miaka mungi ijayo.

Alisema kwa muda wa miezi sita watakuwa chini ya uwangalizi wa kampuni yake pale inapo tokea tatizo watarehebisha bure ilabaada ya hapo itakuwa juu yawizara husika.

Comments