Zanzibar ina wafanyakazi 1026 wa kigeni.

baraza-la-wawakilishiSerikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema haitatoa nafasi za ajira kwa raia wa kigeni  wala kibali bila ya sifa na vigezo maalum wala  hakuna muajiri anaeruhusiwa kuajiri  mfanyakazi wa kigeni isipokuwa pale patakapo kosekana raia Mtanzania mwenye sifa  zitakazotakiwa kujaza nafasi.

Akijibu swali la Mwakilishi wa Jimbo la Jang’ombe Abdalla Maulid Diwani Naibu Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto Shadia Mohammed Suleiman
amesema katika utaratibu wa kawaida muajiri anapaswa  kutangaza nafasi za ajira kupitia  vyombo vya habari na iwapo hakupatikana mwananchi mwenye sifa zilizotajwa muajiri  anaruhusika  kuajiri mfanyakazi wa kigeni na miongozni mwa sifa  ni kiwango cha elimu, ujuzi na uzoefu katika kazi  husika.

Amesema wafanyakazi wa kigeni huajiriwa pale tu sifa kwa nafasi zinazotakiwa kujazwa na wazanzibar  wamekosekana  sifa hizo kwa mujibu wa sheria ya Ajira namba 11 ya mwaka 2005 kifungu 36 kifungu kidogo  cha A na B.

Hata hivyo Naibu Waziri Shadia ametoa wito kwa wazazi na walezi kuwaandaa vyema  vijana wao kielimu kujitahidi kuwasomesha  watoto wao fani mbalimbali  ili kuweza kufikia viwango  vinavyokubalika  na kuingia kwenye  ushindani  katika soko la ajira hasa katika soko la afrika ya mashariki.

Hadi kufikia mwezi machi 2017 Jumla ya wafanyakazi 1026 wa kigeni  wameajiriwa zanzibar  hasa katika sekta ya utalii na miradi maalum ya ushirikiano  baina ya serikali na washirika wa maendeleo katika nyanja mbalimbali.
chanzo:Omar Zanzibar24

Comments