Wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu wamekuwa hawanufaiki na
mifugo yao kutokana na kuibuka kwa kundi la wizi wa mifugo nyakati za
usiku.
Wakizungumza na Zanzibar24 Mwananchi Mwashamba Juma na Sheha wa
Shehia hiyo Khatib Ame wamesema mbali na uwepo wa askari jamii lakini
wanashindwa kuwadhibiti wezi kutokana na zana ndogo wanazotumia wakati
wa kutekeleza wajibu wao.
”mwanzo kulikua na tatizo la wizi wa kuku, lakini baada ya
kuwaekea mtego tulifanikiwa kumkamata mwizi mmoja lakini kwa sasa
kumejitokeza wizi wa mifugo ikiwemo mbuzi, ukiamka asubuhi unakuta
washaibiwa na washachinjwa na wanakuachia vichwa. Hakika hili jambo
linatusikitisha sana” Wamesema wananchi hao.
Wametowa wito kwa Viongozi wa Shehia hiyo kuandaa utaratibu wa kuwapa
mafunzo ya ulinzi askari jamii waliopo ili waweze kupambana na wezi hao
wanaorejesha nyuma maendeleo ya wanakijiji.
chanzo:Zanzibar24.
Comments