
Akiwasilisha hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya Fedha kwa
mwaka 2017/2018 katika kikao cha baraza la wawakilishi Waziri wa wizara
hiyo Balozi Ali Adeid Karume amesema kipaumbele hicho kimepanga
kuanza ujenzi wa barabara ya bububu, mahonda hadi mkokotoni yenye urefu
wa 31.
Aidha amesema mbali na barabara hiyo kipaumbele hicho pia kitajenga
barabara ya koani jumbi yenye urefu wa kilomita 6.3, ujenzi wa barabara
ya wete chake yenye urefu wa kilomita 22 pamoja na ujenzi wa barabara ya
ole kengeje yenye urefu wa kilomita 35.
Hata hivyo amesema katika kuzitekeleza ahadi za Rais wa Zanzibar juu
ya ujenzi wa barabara mbalimbali kipaumbele hicho pia kimekusudia
kutengeneza madaraja yote yaliyoathirika na mvua za masika ikiwemo
changaweni,kiwani,kuugoni,mwanakwerekwe,pujini,kipapo na kibonde mzungu.
Akizungumzia sekta ya Usafirishaji Balozi Karume amesema Serikali
imekusudia kununua meli mpya mbili za mafuta na abiria na boti ndogo za
kusafirishia abiria katika maeneo ya visiwa vidogo vidogo ili
kuwaondolea wananchi usumbufu wa usafiri wanaokaa visiwani humo.
Sambamba na hayo amesema wizara itahakikisha inaimarisha ulinzi na
usalama wa baharini kwa kununua boti nne za doria ambazo zitafanya kazi
kwenye ukanda wa pwani wa Zanzibar kwa lengo la kuwadhibiti wahalifu
hususani waingizaji wa biashara za magendo.
chanzo: Zanzibar24
Comments