Waziri wa Fedha: Zanzibar imepunguza kupokea misaada kutokana na kuimarika kwa vyanzo vya mapato vya ndani.

Akizungumza katika maadhimisho ya wiki ya Mlipa kodi ilioandaliwa na
ZRB amesema hatua hiyo imekuja baada ya wafanyakazi kuwa na mwamko wa
kulipa kodi kwa hiari ambapo imesaidia ukuwaji wa Uchumi.
Amesema mwaka hadi mwaka serikali inaimarisha vyanzo vyake vya ndani
na kupelekea kuweza kujitegemea yenyewe bila ya kutegemea misaada ya
wahisani.
Amesema matatizo yaliopo katika jamii ikiwemo ukosefu wa vitendea
kazi kwa wananfunzi yanatokana na baadhi ya Taasisi za Serikali na
wafanyabiashara kukwepa kulipa kodi kwa wakati.
Aidha ametoa wito kwa wafanyakazi wa taasisi zinzokusanya mapato ZRB
na TRA kufanya kazi kwa uadilifu ili kuengeza ufanisi mzuri katika kazi
zao pamoja na kuwacha tabia ya kutoa misamaha kwa wakwepa kodi pamoja na
kuacha kutoa mizigo wakati wa usiku.
Jumla ya Bilioni mia nane zinatarajiwa kukusanywa kwa walipa kodi
katika kipindi cha mwaka 2017/2018 ambapo malengo yataweza kufikiwa.
chanzo:Zanzibar24.
Comments