Wawili waliopotea waokotwa wakiwa washafariki.

Wavuvi wawili kati ya sita waliozama na kupotea baharini huko Tumbatu kwa zaidi ya siku 4, wameokotwa wakiwa wameshafariki Dunia.

Wavuvi hao walipotea baada ya boti yao kukumbwa na upepo uliopelekea kuzama, waliokotwa katika maeneno tofauti katika mkoa wa Kaskazini Unguja.

Kamanda wa polisi Mkoa wa Kaskazini Unguja Hasina Ramadhan Tawfiq amewataja waliofariki kuwa ni Juma Omar Haji mwenye umri wa 42 aliyeokotwa pwani ya renco nungwi wilaya ya kaskazini A Unguja na Haji Ngwali Sheha mwenye umri wa miaka 47aliyeokotwa katika pwani ya Mwambale wilaya ya kaskazini A.


Aidha wavuvi wa nne kati ya sita walipatikana wakiwa hai na tayari wamepatiwa matibabu na hali zao zinaendelea vizuri.
chanzo: zanzibar24.

Comments