
Wakizungumza wakati wakichangia hoja za bajeti ya wizara ya kazi
Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto katika kikao cha baraza la
wawakilishi Wanu Hafidh Ameir, Asha Abdalla Mussa na Hassan Khamis
Hafidh wamesema, serikali iangalie kwa kina bajeti iliyotenga kabla
haijapitishwa kuwa haitoshelezi kwani kesi za udhalilishaji zina kazi
kubwa katika kufatilia na inahitajika Fedha za kutosha katika
kukabiliana na vitendo hivyo.
Wamesema jamii sasa inakosa imani na serikali kwani kila siku
vitendo vya udhalilishaji vimekuwa vinashamiri bila ya kupatiwa ufumbuzi
kwani kesi zinazofikishwa katika vyombo vya sheria hadi kupatiwa hukumu
ni chache kuliko zinazobakia.
Aidha wamesema vitendo vya udhalilishaji vimekua vikiharibu taswira
ya Zanzibar hivyo serikali lazima itowe hukumu kali kwa wanaotenda
hayo ili kutoa fundisho kwa watu hao.
Hata hivyo wamesema njia ya kumaliza matatizo hayo lazima serikali
itenge pesa za kutosha kwa kitengo kinachofatilia kesi hizo na kuondoa
dhana za utengemezi kutoka kwa wafadhili kwa jambo hilo.
chanzo:Zanzibar24
Comments