Wawakilishi waiomba Serikali kuengeza wataalamu katika sekta ya ujenzi wa Barabara.

baraza-la-wawakilishiKamati ya Ardhi na mawasiliano ya baraza la wawakilishi  imeiomba serikali ya mapinduzi ya Zanzibar kuengeza wataalamu katika sekta ya ujenzi wa Barabara ili kujengwa Barabara zenye ubora na viwango vinavyo takiwa.

Akiwasilisha hutuba ya Maoni ya Kamati hiyo kuhusu makadirio ya Mapato na Matumizi ya wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na usafirishaji kwa mwaka wa Fedha 2017/18 , Makamo mwenyekiti wa Kamati hiyo Suleiman Sarhan Saidi amesema licha ya mafanikio makubwa juu ya kukamilika kwa barabara mbalimbali lakini bado barabara hizo hazina viwango.


Aidha mbali na tatizo hilo idara ya ujenzi na Utunzaji wa Barabara imekabiliwa na matatizo mbalimbali ikiwemo ukosefu wa vifaa vya kutendea kazi , uchakavu wa mitambo ya kutengenezea lami jambo linalopelekea barabara zinazojengwa kuhatarisha maisha ya wananchi hususan katika kipindi cha mvua.

Hata hivyo amesema ili kuondowa matatizo hayo ni vyema kwa serikali kutenga bajeti ya utunzaji na Matengenezo ya Barabara ili kuweza kuzifanyia matengenezo barabara ambazo zipo katika hali mbaya licha nya kuwa hazijapangwa kutengenezwa katika mwaka wa fedha 2017/2018.
chanzo:Zanzibar24

Comments