
Kamanda Moh’d Ali wa KMKM amesema wakati walipokuwa wanaendelea na
doria zao za kawaida ndipo walikishuhudia chombo ambacho kimepakia
wavuvi hao kinazama na ndipo walipoenda kuwaokoa na kufanikiwa kuwapata
wote wakiwa salama.
Nae nahodha wa chombo hicho Antony Mkaringa Mtama alisema chanzo cha
ajali hiyo ni upepeo mkali ambao uliyombisha chombo hicho kuyumba na
kukisababishia kuzama.
Wavuvi walionusurika kufa ni pamoja na Said Abdallah Fadhili Mo’d
Haji, Fokas Mtata, Mtumweni na wawili ni abiria ambao bado
hawajatambulika majina yao.
chanzo: zanzibar24.
Comments