Watuhumiwa 12 wa mauaji Pwani wasakwa.

JESHI la Polisi limeanza kuwasaka watuhumiwa 12 wa mauaji ya Polisi na raia katika wilaya za Mkuranga, Kibiti na Rufiji, mkoani Pwani, baada ya kuwabaini kutokana na vyanzo mbalimbali.

Aidha, katika kukoleza kasi ya msako huo, jeshi hilo limetangaza kutoa dau nono la Sh milioni 5 kwa watakaofanikisha kukamatwa kwa watuhumiwa hao. Hayo yalibainika jana mjini hapa kupitia taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Onesmo Lyanga.


Amewataja watuhumiwa hao kuwa ni pamoja na Abdulshakur Makeo aliyetajwa kuwa ni mwanzishi wa harakati za mauaji Ikwiriri, wilayani Rufiji. Wengine ni Faraj Nangalava, Anaf Kapera pia anafahamika zaidi kama Kapelo, Said Ngunde, Omar Matimbwa, Shaaban Kinyangulia, Haji Ulatule, Ally Ulatule, Hassan Uponda, Rashid Mtulula, Shehe Hassan Mzuzuri na Hassan Njame

Zaidi ya  watu 31 wamepoteza maisha, wakiwemo viongozi na makada wa chama tawala, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutokana na mauaji yanayoendelea Mkoani Pwani.
chanzo:zanzibar24.

Comments