Wateja wa FBME Zanzibar wapata wasiwasi juu ya hatma yao.

ufuatia Benki Kuu ya Tanzania (BOT) kuifutia  leseni ya biashara Benki ya FBME Baadhi ya wateja wa Benki hiyo hapa Zanzibar wameonyesha wasiwasi wao juu ya hatma ya akiba zao zilizopo katika Benki hiyo.
Wakizungumza na mwandishi wetu baadhi ya wateja hao wamesema tokea kufungwa kwa banki hiyo  hakuna taarifa  yoyote waliyopewa kuhusu kupatikana kwa fedha zao.

Kwa upande wake Mshauri Bodi ya Bima ya Amana Rashid Mrutu ambayo imepewa dhamana ya kuwa mfilisi wa Benki hiyo amewataka wadai na wadaiwa  kuwa wavumilivu  wakati Mfilisi akiandaa utaratibu wa kushughulikia  stahiki zao.
Uamuzi huo wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT)  ya kuifutia lessen Benki hiyo ya FBME umetolewa baada ya hukumu ya kesi ya utakatishaji fedha iliyokuwa ikiikabili benki hiyo kutolewa.
Itakumbukwa mwaka 2014, Mtandao wa Kudhibiti Uhalifu wa Masuala ya Fedha (FinCEN) wa Marekani uliitaja FBME kuwa taasisi inayojihusisha na utakatishaji fedha hivyo kuizuia kutoa huduma nchini humo.
chanzo:zanzibar24.

Comments