Hayo yalisemwa Bagamoyo na Kaimu Katibu mkuu wa Umoja wa Vijana
(UVCCM) Taifa Shaka Hamdu Shaka wakati wa ziara yake kufuatilia uhai wa
chama na utekelezaji wa Ilani wilayani humo na mkoa wa Pwani.
Shaka alisema kuwa kumekuwa na uhaba wa maeneo kwa ajili ya ujenzi wa
taasisi za elimu hasa mashule ambapo miaka ijayo hakutakuwa na maeneo
kabisa kwa ajili ya ujenzi hali ambayo itasababisha ujenzi huo kuwa
mgumu.
“Tuzungumza na Waziri wa Elimu ili aweze kutoa mwongozo wa ujenzi wa
aina hiyo kwa ajili ya maeneo ya shule ambapo kuna idadi kubwa ya watoto
ambao watakuwa wakihitaji kupata elimu ambapo kwa sasa imeonekana kuna
uhaba wa maeneo ya ujenzi wa shule hasa za msingi,” alisema Shaka.
Alisema kuwa kwa sasa kumekuwa na mwamko mkubwa wa wananchi
kuwapeleka watoto wao shule hali ambayo imesababisha kuhitajika ujenzi
wa majengo mengi ya taasisi za elimu.
Kaimu Katibu mkuu akiwa ziarani Bagamoyo alitembelea mradi wa
maendeleo wa ujenzi wa nyumba ya watumishi kwenye zahanati ya Kaole
pamoja na ujenzi wa madarasa na choo kwenye shule ya Msingi Muungano na
jana alitarajiwa kutembelea Jimbo la Chalinze
chanzo:Habarileo.
Comments